Zaburi 85:1-13

  • Sala ya kuomba warudishwe

    • Mungu atawaambia washikamanifu wake kuhusu amani (8)

    • Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu (10)

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+ 85  Ee Yehova, umeionyesha kibali nchi yako;+Uliwarudisha watu wa Yakobo waliokuwa wametekwa.+   Umelisamehe kosa la watu wako;Ulisamehe* dhambi yao yote.+ (Sela)   Uliizuia ghadhabu yako yote;Uliiacha hasira yako kali.+   Turudishe,* Ee Mungu wa wokovu wetu,Na uache kutukasirikia.+   Je, utatughadhibikia milele?+ Je, utaendelea kukasirika kizazi baada ya kizazi?   Je, hutatuhuisha tenaIli watu wako washangilie kwa sababu yako?+   Ee Yehova, tutendee kwa upendo mshikamanifu,+Nawe utupe wokovu wako.   Nitasikiliza jambo ambalo Mungu wa kweli Yehova anasema,Kwa maana atawaambia watu wake kuhusu amani,+ washikamanifu wake,Lakini wasianze tena kujiamini kupita kiasi.+   Kwa hakika wokovu wake uko karibu na wale wanaomwogopa,+Ili utukufu wake ukae katika nchi yetu. 10  Upendo mshikamanifu utakutana na uaminifu;Uadilifu utabusiana na amani.+ 11  Uaminifu utachipuka duniani,Na uadilifu utatazama chini kutoka mbinguni.+ 12  Naam, Yehova atatoa kilicho chema,*+Na nchi yetu itazaa mavuno yake.+ 13  Uadilifu utatembea mbele zake+Na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Uliifunika.”
Au “Tukusanye tena.”
Au “ufanisi.”