Zaburi 87:1-7

  • Sayuni, jiji la Mungu wa kweli

    • Waliozaliwa Sayuni (4-6)

Muziki wa wana wa Kora.+ Wimbo. 87  Msingi wa jiji lake uko katika milima mitakatifu.+   Yehova anapenda malango ya Sayuni+Kuliko mahema yote ya Yakobo.   Mambo matukufu yanasemwa kukuhusu, Ee jiji la Mungu wa kweli.+ (Sela)   Nitamhesabu Rahabu+ na Babiloni kuwa kati ya wale wanaonijua* mimi;Tazama, Ufilisti na Tiro, pamoja na Kushi. Itasemwa hivi: “Huyu alizaliwa humo.”   Na kuhusu Sayuni itasemwa: “Kila mtu alizaliwa humo.” Na Aliye Juu Zaidi atamwimarisha kabisa.   Yehova atatangaza hivi atakapoyaandikisha mataifa: “Huyu alizaliwa humo.” (Sela)   Waimbaji+ na wale wanaocheza dansi za mzunguko+ watasema: “Chemchemi zangu zote zimo ndani yako.”*+

Maelezo ya Chini

Au “wanaonitambua.”
Au “Kwangu mimi, wewe ni chanzo cha vitu vyote.”