Zaburi 88:1-18

  • Sala ya kuomba ulinzi dhidi ya kifo

    • “Uhai wangu uko kwenye kingo za Kaburi” (3)

    • ‘Kila asubuhi ninasali kwako’ (13)

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ Kwa kiongozi; kwa mtindo wa Mahalathi,* uimbwe kwa zamu. Maskili* ya Hemani+ Mwezra. 88  Ee Yehova, Mungu wa wokovu wangu,+Wakati wa mchana ninalia kwa sauti,Na usiku ninakuja mbele zako.+   Sala yangu na ikufikie,+Tega sikio lako* usikie kilio changu cha kuomba msaada.+   Kwa maana nafsi* yangu imejaa msiba,+Na uhai wangu uko kwenye kingo za Kaburi.*+   Tayari nimehesabiwa miongoni mwa wale wanaoshuka shimoni;*+Nimekuwa mtu asiye na uwezo wowote,*+   Aliyeachwa kati ya watu waliokufaKama waliouawa wanaolala kaburini,Ambao huwakumbuki tenaNa ambao wametengwa mbali na utunzaji* wako.   Umeniweka katika shimo lenye kina kirefu sana,Sehemu zenye giza, shimo kubwa.*   Ghadhabu yako inanilemea sana,+Nawe unanilemea kwa mawimbi yako yenye nguvu. (Sela)   Umewafukuza rafiki zangu mbali sana nami;+Umenifanya niwe kitu kinachowachukiza. Nimenaswa na siwezi kutoroka.   Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya mateso yangu.+ Ee Yehova, ninakulilia mchana kutwa;+Ninakunyooshea mikono yangu. 10  Je, utawatendea maajabu waliokufa? Je, wale waliokufa ambao hawana uwezo wanaweza kuinuka na kukusifu?+ (Sela) 11  Je, upendo wako mshikamanifu utatangazwa kaburini,Na uaminifu wako mahali pa maangamizi?* 12  Je, maajabu yako yatajulikana gizaniAu uadilifu wako katika nchi ya waliosahauliwa?+ 13  Lakini bado ninakulilia unisaidie, Ee Yehova,+Kila asubuhi sala yangu inakufikia.+ 14  Kwa nini, Ee Yehova, unanikataa?*+ Kwa nini unanificha uso wako?+ 15  Tangu nilipokuwa kijana,Nimeteseka nami niko karibu kuangamia;+Nimekufa ganzi kwa sababu ya mambo yanayotisha unayoruhusu yanipate. 16  Hasira yako inayowaka inanilemea;+Vitisho vyako vinaniangamiza. 17  Vinanizunguka mchana kutwa kama maji;Vinanizingira ili kunibana pande zote.* 18  Umewafukuza rafiki zangu na wenzangu mbali sana nami;+Giza limekuwa mwenzangu.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “Inama chini na unisikilize.”
Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “mtu asiye na nguvu.”
Au “kaburini.”
Tnn., “mkono.”
Au “abiso.” Angalia Kamusi.
Au “katika Abadoni.”
Au “unaikataa nafsi yangu.”
Au labda, “Vinanizingira vyote kwa pamoja.”