Zaburi 89:1-52

  • Kuimba kuhusu upendo mshikamanifu wa Yehova

    • Agano pamoja na Daudi (3)

    • Uzao wa Daudi utadumu milele (4)

    • Mtiwa-mafuta wa Mungu amwita Yeye “Baba” (26)

    • Agano la Daudi ni hakika (34-37)

    • Mwanadamu hawezi kuponyoka Kaburi (48)

Maskili.* Wa Ethani+ Mwezra. 89  Nitaimba kuhusu jinsi Yehova anavyoonyesha upendo mshikamanifu milele. Kwa kinywa changu ninavitangazia vizazi vyote uaminifu wako.   Kwa maana nimesema: “Upendo mshikamanifu utajengwa* milele,+Nawe umeuimarisha kabisa uaminifu wako mbinguni.”   “Nimefanya agano pamoja na yule niliyemchagua;+Nimemwapia Daudi mtumishi wangu:+   ‘Nitauimarisha kabisa uzao wako*+ milele,Nami nitakijenga kiti chako cha ufalme kwa vizazi vyote.’”+ (Sela)   Mbingu zinasifu maajabu yako, Ee Yehova,Naam, uaminifu wako katika kutaniko la watakatifu.   Kwa maana ni nani mbinguni anayeweza kulinganishwa na Yehova?+ Ni nani miongoni mwa wana wa Mungu+ aliye kama Yehova?   Mungu anaogopwa katika baraza* la watakatifu;+Yeye ni mtukufu na mwenye kuogopesha kwa wote wanaomzunguka.+   Ee Yehova Mungu wa majeshi,Ni nani aliye na nguvu kama wewe, Ee Yah?+ Uaminifu wako unakuzunguka.+   Unautawala msukosuko wa bahari;+Mawimbi yake yanapoinuka, unayatuliza.+ 10  Umemponda Rahabu+ kama mtu aliyeuawa.+ Kwa mkono wako wenye nguvu umewatawanya maadui wako.+ 11  Mbingu ni zako, na dunia ni yako;+Nchi inayozaa na vinavyoijaza+—umeviumba. 12  Kaskazini na kusini—uliziumba;Tabori+ na Hermoni+ hulisifu kwa shangwe jina lako. 13  Mkono wako una uwezo;+Mkono wako una nguvu;+Mkono wako wa kuume umekwezwa.+ 14  Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chako cha ufalme;+Upendo mshikamanifu na uaminifu husimama mbele zako.+ 15  Wenye furaha ni watu wanaojua kelele za shangwe.+ Ee Yehova, wanatembea katika nuru ya uso wako. 16  Wanashangilia mchana kutwa kwa sababu ya jina lako,Na kwa sababu ya uadilifu wako wanakwezwa. 17  Kwa maana wewe ni utukufu wa nguvu zao,+Na kwa kibali chako nguvu zetu zinakwezwa.*+ 18  Kwa maana ngao yetu ni ya Yehova,Mfalme wetu ni wa Mtakatifu wa Israeli.+ 19  Wakati huo uliwaambia hivi washikamanifu wako katika maono: “Nimempa nguvu aliye hodari;+Nimemkweza aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu.+ 20  Nimempata Daudi mtumishi wangu;+Kwa mafuta yangu matakatifu nimemtia mafuta.+ 21  Mkono wangu utamtegemeza,+Na mkono wangu utamwimarisha. 22  Hakuna adui atakayemtoza ushuru,Na hakuna mwovu atakayemkandamiza.+ 23  Nitawavunja maadui wake vipandevipande kutoka mbele yake+Na kuwaangamiza wale wanaomchukia.+ 24  Uaminifu wangu na upendo wangu mshikamanifu uko pamoja naye,+Na katika jina langu nguvu zake zitakwezwa.* 25  Nitauweka mkono wake* juu ya bahariNa mkono wake wa kulia juu ya mito.+ 26  Atasema kwa sauti: ‘Wewe ni Baba yangu,Mungu wangu na Mwamba wa wokovu wangu.’+ 27  Nami nitamfanya kuwa mzaliwa wa kwanza,+Aliye juu zaidi kati ya wafalme wa dunia.+ 28  Nitadumisha upendo wangu mshikamanifu kumwelekea milele,+Na agano langu nililofanya pamoja naye halitavunjika kamwe.+ 29  Nitauimarisha uzao wake* mileleNa kukifanya kiti chake cha ufalme kidumu kama mbingu.+ 30  Wanawe wakiiacha sheria yanguNa wasipotembea kulingana na maagizo yangu,* 31  Wakizivunja sheria zanguNa wasiposhika amri zangu, 32  Basi nitaadhibu uasi wao* kwa fimbo+Na kosa lao kwa viboko. 33  Lakini sitaacha kamwe kumtendea kwa upendo wangu mshikamanifu+Wala sitakosa kutimiza ahadi yangu.* 34  Sitavunja agano langu+Wala kubadili maneno yaliyosemwa na midomo yangu.+ 35  Nimeapa katika utakatifu wangu, mara moja kwa wakati wote;Sitamwambia Daudi uwongo.+ 36  Uzao wake utadumu* milele;+Kiti chake cha ufalme kitadumu kama jua mbele zangu.+ 37  Kama mwezi, kitaimarishwa kabisa mileleKama shahidi mwaminifu angani.” (Sela) 38  Lakini wewe mwenyewe umemtupa mbali na kumkataa;+Umemkasirikia sana mtiwa-mafuta wako. 39  Umelikataa kwa dharau agano ulilofanya na mtumishi wako;Umelichafua* taji lake kwa kulitupa ardhini. 40  Umezivunja kuta zake zote za mawe;*Umezifanya ngome zake kuwa magofu. 41  Wote wanaopita karibu naye wamempora;Yeye ni shutuma kwa jirani zake.+ 42  Umewapa ushindi wapinzani wake;*+Umewafanya maadui wake wote washangilie. 43  Pia umeusukuma nyuma upanga wake,Na kumfanya ashindwe vitani. 44  Umekomesha fahari yakeNa kukitupa ardhini kiti chake cha ufalme. 45  Umefupisha siku zake za ujana;Umemvisha aibu. (Sela) 46  Ee Yehova, utaendelea kujificha mpaka lini? Utajificha milele?+ Je, ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto? 47  Kumbuka jinsi maisha yangu yalivyo mafupi!+ Je, uliwaumba wanadamu wote bila kusudi? 48  Ni mwanadamu gani anayeweza kuishi na asione kifo kamwe?+ Je, anaweza kujiokoa mwenyewe* kutoka katika nguvu za Kaburi?* (Sela) 49  Yako wapi matendo yako ya zamani ya upendo mshikamanifu, Ee Yehova,Ambayo ulimwapia Daudi katika uaminifu wako?+ 50  Kumbuka, Ee Yehova, dhihaka ambazo watumishi wako wanavurumishiwa;Jinsi ninavyolazimika kuvumilia* dhihaka za mataifa yote; 51  Jinsi ambavyo maadui wako wamevurumisha matusi, Ee Yehova;Jinsi ambavyo wameitukana kila hatua ya mtiwa-mafuta wako. 52  Yehova na asifiwe milele. Amina na Amina.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “utadumu.”
Tnn., “Nitaiimarisha kabisa mbegu yako.”
Au “kusanyiko.”
Tnn., “pembe yetu inakwezwa.”
Tnn., “pembe yake itakwezwa.”
Au “Nitaweka mamlaka yake.”
Tnn., “Nitaiimarisha mbegu yake.”
Au “hukumu zangu.”
Au “kutotii kwao.”
Tnn., “Wala kuwa mwongo kuhusu uaminifu wangu.”
Tnn., “Mbegu yake itadumu.”
Au “Umelitia unajisi.”
Au “Umeyavunja mabanda yake yote ya mawe.”
Tnn., “Umeuinua juu mkono wa kulia wa maadui wake.”
Au “kuiokoa nafsi yake.”
Tnn., “mkono wa Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “kubeba kifuani mwangu.”