Zaburi 9:1-20

  • Kutangaza kazi za Mungu zinazostaajabisha

    • Yehova ni kimbilio salama (9)

    • Kulijua jina la Mungu humaanisha kumtumaini yeye (10)

Kwa kiongozi; juu ya Muth-labeni.* Muziki wa Daudi. א [Aleph] 9  Nitakusifu, Ee Yehova, kwa moyo wangu wote;Nitasimulia kuhusu kazi zako zote zinazostaajabisha.+   Nitafurahi na kushangilia kwa sababu yako;Nitaliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi.+ ב [Beth]   Maadui wangu wanapokimbia,+Watajikwaa na kuangamia kutoka mbele zako.   Kwa maana unatetea njia yangu ya haki;Unaketi kwenye kiti chako cha ufalme ukihukumu kwa uadilifu.+ ג [Gimel]   Umeyakemea mataifa+ na kuwaangamiza waovu,Na hivyo kulifuta jina lao milele na milele.   Maadui wameangamizwa milele;Uliyang’oa majiji yao,Na kumbukumbu lote kuwahusu litatoweka.+ ה [He]   Lakini Yehova ameketi kwenye kiti cha ufalme milele;+Amekiimarisha kabisa kiti chake cha ufalme kwa ajili ya haki.+   Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa;+Atayahukumu mataifa kwa kutoa maamuzi ya uadilifu.+ ו [Waw]   Yehova atakuwa kimbilio salama* kwa wanaokandamizwa,+Kimbilio salama katika nyakati za taabu.+ 10  Wale wanaolijua jina lako watakutumaini wewe;+Hutawaacha kamwe wale wanaokutafuta, Ee Yehova.+ ז [Zayin] 11  Mwimbieni sifa Yehova, anayekaa Sayuni;Tangazeni matendo yake miongoni mwa mataifa.+ 12  Kwa maana Yule anayelipiza kisasi kwa ajili ya damu yao anawakumbuka;+Hatasahau kilio cha wanaoteseka.+ ח [Heth] 13  Nionyeshe kibali, Ee Yehova; angalia ninavyoteswa na wale wanaonichukia,Wewe unayeniinua kutoka katika malango ya kifo,+ 14  Ili nitangaze katika malango ya binti ya Sayuni matendo yako yanayostahili sifa,+Na kushangilia kwa sababu ya matendo yako ya wokovu.+ ט [Teth] 15  Mataifa yamezama chini katika shimo walilochimba;Mguu wao wenyewe umenaswa katika wavu waliouficha.+ 16  Yehova anajulikana kwa hukumu anazotekeleza.+ Mwovu amenaswa katika kazi za mikono yake mwenyewe.+ Higayoni.* (Sela) י [Yod] 17  Waovu watageuka na kuelekea Kaburini,*Mataifa yote yanayomsahau Mungu. 18  Lakini maskini hawatasahauliwa daima;+Wala tumaini la wapole halitapotea kamwe.+ כ [Kaph] 19  Inuka, Ee Yehova! Usiache mwanadamu anayeweza kufa ashinde. Mataifa na yahukumiwe mbele zako.*+ 20  Wapige kwa woga, Ee Yehova,+Acha mataifa yajue kwamba wao ni wanadamu tu wanaoweza kufa. (Sela)

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “Nitalipigia muziki.”
Au “kilele salama.”
Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mbele za uwepo wako.”