Zaburi 90:1-17

  • Mungu wa milele na mwanadamu anayeishi kwa muda mfupi

    • Miaka elfu moja ni kama jana (4)

    • Mwanadamu anaishi miaka 70-80 (10)

    • “Tufundishe jinsi ya kuhesabu siku zetu” (12)

Sala ya Musa, mtu wa Mungu wa kweli.+ 90  Ee Yehova, umekuwa makao yetu*+ katika vizazi vyote.   Kabla milima haijazaliwaAu kabla hujaiumba* dunia na nchi inayozaa,+Tangu milele hadi milele, wewe ni Mungu.+   Unamfanya mwanadamu anayeweza kufa arudi mavumbini;Unasema: “Rudini, enyi wanadamu.”+   Kwa maana miaka elfu moja machoni pako ni kama siku ya jana ambayo tayari imepita,+Kama kesha moja tu la usiku.   Unawafagilia mbali;+ wanakuwa kama usingizi tu;Asubuhi, wao ni kama majani yanayochipuka.+   Asubuhi yanachanua maua na kusitawi,Lakini ifikapo jioni yamenyauka na kukauka.+   Kwa maana tumemezwa na hasira yako+Na kutishwa na ghadhabu yako.   Unayaweka makosa yetu mbele zako;*+Siri zetu zinafichuliwa na nuru ya uso wako.+   Siku zetu zinadidimia* kwa sababu ya ghadhabu yako;Na miaka yetu hufikia kikomo kama mnong’ono.* 10  Urefu wa maisha yetu ni miaka 70,Au miaka 80+ ikiwa mtu ana nguvu za pekee.* Lakini imejaa taabu na huzuni;Nayo hupita haraka, nasi hutokomea.+ 11  Ni nani anayeweza kuelewa nguvu za hasira yako? Ghadhabu yako ni kubwa kama hofu unayostahili kuonyeshwa.+ 12  Tufundishe jinsi ya kuhesabu siku zetu+Ili tupate moyo wa hekima. 13  Rudi, Ee Yehova!+ Hali hiyo itadumu mpaka lini?+ Wahurumie watumishi wako.+ 14  Tushibishe asubuhi kwa upendo wako mshikamanifu,+Ili tupaze sauti kwa shangwe na kushangilia+ siku zetu zote. 15  Tufanye tushangilie kulingana na siku ambazo umetutesa,+Kwa kadiri ya miaka mingi tuliyopata msiba.+ 16  Watumishi wako na waone utendaji wako,Na wana wao waone fahari yako.+ 17  Kibali chako, Ee Yehova Mungu wetu, na kiwe juu yetu;Na uifanikishe* kazi ya mikono yetu. Naam, ifanikishe* kazi ya mikono yetu.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “kimbilio letu.”
Au “hujatokeza kama kwa uchungu wa kuzaa.”
Au “Unajua makosa yetu.”
Au “Maisha yetu yanadidimia.”
Au “kupiga kite.”
Au “kwa sababu ya uwezo wa pekee.”
Au “uimarishe kabisa.”
Au “iimarishe kabisa.”