Zaburi 91:1-16

  • Ulinzi mahali pa siri pa Mungu

    • Kuokolewa kutoka kwa mwindaji wa ndege (3)

    • Kukimbilia chini ya mabawa ya Mungu (4)

    • Usalama hata elfu moja wakianguka (7)

    • Malaika waagizwa kutoa ulinzi (11)

91  Yeyote anayekaa mahali pa siri pa Aliye Juu Zaidi+Ataishi katika kivuli cha Mweza-Yote.+   Nitamwambia Yehova: “Wewe ni kimbilio langu na ngome yangu,+Mungu wangu ninayemtumaini.”+   Kwa maana atakuokoa usinaswe na mtego wa mwindaji wa ndege,Kutoka kwa ugonjwa wa kuambukiza unaoangamiza.   Kwa manyoya yake atakufunika,Nawe utapata kimbilio chini ya mabawa yake.+ Uaminifu wake+ utakuwa ngao kubwa+ na ukuta wa ulinzi.*   Hutaogopa vitisho vya usiku,+Wala mshale unaoruka mchana,+   Wala ugonjwa wa kuambukiza unaonyemelea gizani,Wala maangamizi yanayoharibu wakati wa adhuhuri.   Elfu moja wataanguka kando yakoNa elfu kumi mkono wako wa kulia,Lakini hayatakukaribia wewe.+   Utayaona tu kwa macho yakoUnaposhuhudia adhabu* ya waovu.   Kwa sababu ulisema: “Yehova ni kimbilio langu,” Umemfanya Aliye Juu Zaidi kuwa makao* yako;+ 10  Hutapatwa na msiba,+Na hakuna pigo litakalokaribia hema lako. 11  Kwa maana atawaagiza malaika zake+ kukuhusu wewe,Ili kukulinda katika njia zako zote.+ 12  Watakubeba mikononi mwao,+Ili mguu wako usigonge jiwe.+ 13  Utamkanyaga mwanasimba na swila;Utamkanyagia chini simba mwenye manyoya marefu shingoni na nyoka mkubwa.+ 14  Mungu alisema: “Kwa sababu ananipenda,* nitamwokoa.+ Nitamlinda kwa sababu analijua* jina langu.+ 15  Ataniita, nami nitamjibu.+ Nitakuwa pamoja naye katika taabu.+ Nitamwokoa na kumtukuza. 16  Nitamshibisha kwa maisha marefu,+Nami nitamfanya aone matendo yangu ya wokovu.”*+

Maelezo ya Chini

Au “boma.”
Tnn., “malipo.”
Au labda, “ngome; kimbilio.”
Tnn., “amejiunga nami.”
Au “analitambua.”
Au “aone wokovu kutoka kwangu.”