Zaburi 92:1-15

  • Yehova akwezwa milele

    • Kazi zake kuu na mawazo yake yenye kina (5)

    • ‘Waadilifu watasitawi kama mti’ (12)

    • Waliozeeka wataendelea kunawiri (14)

Muziki. Wimbo wa siku ya Sabato. 92  Ni vema kukushukuru, Ee Yehova+Na kuliimbia sifa* jina lako, Ee Uliye Juu Zaidi,   Kutangaza upendo wako mshikamanifu+ asubuhiNa uaminifu wako nyakati za usiku,   Kwa kinanda cha nyuzi kumi na kwa udi,Kwa sauti tamu ya kinubi.+   Kwa maana umenifanya nishangilie, Ee Yehova, kwa sababu ya matendo yako;Kwa sababu ya kazi za mikono yako ninapaza sauti kwa shangwe.   Jinsi kazi zako zilivyo kuu, Ee Yehova!+ Jinsi mawazo yako yalivyo na kina sana!+   Mtu yeyote asiyetumia akili hawezi kuyajua;Na hakuna mtu yeyote mjinga anayeweza kuelewa hili:+   Waovu wanapochipuka kama magugu*Na watenda mabaya wote wanapositawi,Ni ili waangamizwe milele.+   Lakini wewe umekwezwa milele, Ee Yehova.   Kwa kweli, watazame maadui wako wakishindwa, Ee Yehova,Tazama jinsi maadui wako watakavyoangamia;Watenda maovu wote watatawanywa.+ 10  Lakini utazikweza nguvu zangu kama za* fahali mwitu;Nitailainisha ngozi yangu kwa mafuta mapya.+ 11  Macho yangu yatawaangalia maadui wangu wakishindwa;+Masikio yangu yatasikia kuhusu kuangamia kwa watu waovu wanaonishambulia. 12  Lakini waadilifu watasitawi kama mtendeNa kuwa wakubwa kama mwerezi kule Lebanoni.+ 13  Wamepandwa katika nyumba ya Yehova;Wanasitawi katika nyua za Mungu wetu.+ 14  Hata wakati wa uzeeni* wataendelea kunawiri;+Wataendelea kuwa na nguvu* na kuwa wabichi,+ 15  Wakitangaza kwamba Yehova ni mnyoofu. Yeye ni Mwamba wangu,+ ambaye hana ukosefu wowote wa uadilifu.

Maelezo ya Chini

Au “kulipigia muziki.”
Au “majani.”
Tnn., “utaikweza pembe yangu kama ya.”
Au “wakiwa na mvi.”
Tnn., “kuwa wanene.”