Zaburi 93:1-5

  • Utawala wa Yehova wenye utukufu

    • “Yehova amekuwa Mfalme!” (1)

    • “Vikumbusho vyako vinategemeka” (5)

93  Yehova amekuwa Mfalme!+ Amevaa adhama;Yehova amevaa nguvu;Huzivaa kama mshipi. Dunia imeimarishwa kabisa;Haiwezi kusogezwa.*   Kiti chako cha ufalme kiliimarishwa kabisa zamani za kale;+Umekuwapo tangu milele.+   Mito imefurika, Ee Yehova,Mito imefurika na kunguruma;Mito inaendelea kufurika na kugonga kwa kishindo.   Ana nguvu kuliko sauti ya maji mengi,Ana nguvu kuliko mawimbi makubwa ya bahari,+Yehova ni mwenye fahari mbinguni.+   Vikumbusho vyako vinategemeka sana.+ Utakatifu unaipamba* nyumba yako nyakati zote,+ Ee Yehova.

Maelezo ya Chini

Au “kutikiswa.”
Au “unaifaa.”