Zaburi 94:1-23

  • Sala ya kuomba Mungu alipize kisasi

    • “Waovu wataendelea mpaka lini?” (3)

    • Kurekebishwa na Yah huleta furaha (12)

    • Mungu hatawaacha watu wake (14)

    • ‘Kutunga matatizo kwa kutumia sheria’ (20)

94  Ee Mungu wa kisasi, Yehova,+Ee Mungu wa kisasi, angaza!   Inuka, Ee Mwamuzi wa dunia.+ Walipe wanachostahili watu wenye kiburi.+   Waovu wataendelea mpaka lini, Ee Yehova,Waovu wataendelea mpaka lini kushangilia?+   Wanaropoka na kuongea kwa kiburi;Watenda dhambi wote wanajigamba kujihusu.   Wanawaponda watu wako, Ee Yehova,+Na kuukandamiza urithi wako.   Wanamuua mjane na mkaaji mgeni,Na kuwaua mayatima.   Wanasema: “Yah haoni;+Mungu wa Yakobo hatambui jambo hilo.”+   Eleweni jambo hili, ninyi msiotumia akili;Ninyi wajinga, ni lini mtakapoonyesha ufahamu?+   Yule aliyetengeneza* sikio, je, hawezi kusikia? Yule aliyeumba jicho, je, hawezi kuona?+ 10  Yule anayeyarekebisha mataifa, je, hawezi kukaripia?+ Yeye Ndiye anayewafundisha watu ujuzi!+ 11  Yehova anajua mawazo ya wanadamu,Ya kwamba ni pumzi tu.+ 12  Mwenye furaha ni mtu unayemrekebisha, Ee Yah,+Unayemfundisha kwa sheria yako,+ 13  Ili kumpa utulivu katika siku za msiba,Mpaka shimo litakapochimbwa kwa ajili ya mwovu.+ 14  Kwa maana Yehova hatawaacha watu wake,+Wala hatautupa urithi wake.+ 15  Kwa maana kwa mara nyingine tena hukumu itakuwa ya uadilifu,Na wote walio wanyoofu moyoni wataifuata. 16  Ni nani atakayeinuka dhidi ya waovu kwa ajili yangu? Ni nani atakayenitetea dhidi ya watenda maovu? 17  Ikiwa Yehova hangekuwa msaidizi wangu,Ningekuwa nimeangamia upesi.*+ 18  Niliposema: “Mguu wangu unateleza,” Upendo wako mshikamanifu, Ee Yehova, uliendelea kunitegemeza.+ 19  Mahangaiko* yaliponilemea,*Ulinifariji na kunibembeleza.*+ 20  Je, kiti cha ufalme* chenye ufisadi kinaweza kuungana naweWakati kinapotunga matatizo kwa kutumia sheria?*+ 21  Wanamshambulia vikali mwadilifu+Na kumhukumu asiye na hatia auawe.*+ 22  Lakini Yehova atakuwa kimbilio langu salama,*Mungu wangu ni mwamba wangu ninaokimbilia.+ 23  Atafanya matendo yao maovu yawarudie.+ Atawaangamiza* kwa uovu wao wenyewe. Yehova Mungu wetu atawaangamiza.*+

Maelezo ya Chini

Tnn., “aliyelipanda.”
Tnn., “nimekaa katika ukimya.”
Au “Mawazo yenye kufadhaisha.”
Au “yalipokuwa mengi ndani yangu.”
Au “Faraja zako ziliibembeleza nafsi yangu.”
Au “watawala; mahakimu.”
Au “kwa kutoa amri.”
Tnn., “Na damu ya asiye na hatia wanaitangaza kuwa na hatia (ovu).”
Au “kilele changu salama.”
Tnn., “Atawanyamazisha.”
Tnn., “atawanyamazisha.”