Zaburi 95:1-11

  • Ibada ya kweli pamoja na utii

    • “Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake” (7)

    • “Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu” (8)

    • “Hawataingia katika pumziko langu” (11)

95  Njooni, na tumshangilie Yehova kwa sauti! Na tumpazie sauti kwa ushindi Mwamba wetu wa wokovu.+   Twendeni mbele zake* tukiwa na shukrani;+Na tuimbe na kumpazia sauti kwa ushindi.   Kwa maana Yehova ni Mungu mkuu,Mfalme mkuu juu ya miungu mingine yote.+   Sehemu zenye kina za dunia zimo mkononi mwake;Vilele vya milima ni vyake.+   Bahari, ambayo aliiumba, ni yake,+Na mikono yake ilitengeneza nchi kavu.+   Njooni, tuabudu na kuinama;Na tupige magoti mbele za Yehova Muumba wetu.+   Kwa maana yeye ni Mungu wetu,Na sisi ni watu wa malisho yake,Kondoo anaowatunza.*+ Leo ikiwa mtaisikiliza sauti yake,+   Msiufanye moyo wenu kuwa mgumu kama mlivyofanya kule Meriba,*+Kama katika siku ya Masa* kule nyikani,+   Mababu zenu waliponijaribu;+Walinipima, ingawa walikuwa wameona matendo yangu.+ 10  Kwa miaka 40 nilichukizwa na kizazi hicho, nikasema: “Wao ni watu wanaopotoka sikuzote katika mioyo yao;Hawajazijua njia zangu.” 11  Kwa hiyo niliapa kwa hasira yangu: “Hawataingia katika pumziko langu.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “mbele za uso wake.”
Tnn., “wa mkono wake.”
Maana yake “Kugombana.”
Maana yake “Kujaribu; Jaribu.”