Zaburi 96:1-13

  • “Mwimbieni Yehova wimbo mpya”

    • Yehova anastahili kusifiwa kuliko wote (4)

    • Miungu ya mataifa ni ubatili (5)

    • Abuduni katika mapambo matakatifu (9)

96  Mwimbieni Yehova wimbo mpya.+ Mwimbieni Yehova, dunia yote!+   Mwimbieni Yehova; lisifuni jina lake. Tangazeni habari njema za wokovu wake siku baada ya siku.+   Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.+   Yehova ni mkuu na anastahili kusifiwa kuliko wote. Anaogopesha kuliko miungu mingine yote.   Miungu yote ya mataifa ni miungu ya ubatili,+Lakini Yehova ndiye aliyeziumba mbingu.+   Mbele zake kuna utukufu* na fahari;+Nguvu na uzuri umo mahali pake patakatifu.+   Mpeni Yehova anachostahili, enyi familia za mataifa,Mpeni Yehova anachostahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+   Mpeni Yehova utukufu ambao jina lake linastahili;+Leteni zawadi na mwingie katika nyua zake.   Mwinamieni* Yehova katika mapambo matakatifu;*Tetemekeni mbele zake, dunia yote! 10  Tangazeni miongoni mwa mataifa: “Yehova amekuwa Mfalme!+ Dunia imeimarishwa kabisa, haiwezi kusogezwa.* Atayahukumu* mataifa kwa haki.”+ 11  Mbingu na zishangilie, dunia na iwe na shangwe;Bahari na ingurume na vitu vyote vinavyoijaza;+ 12  Mashamba na vitu vyote vilivyomo na vishangilie.+ Wakati uleule miti yote ya msituni na ishangilie kwa sauti+ 13  Mbele za Yehova, kwa maana anakuja,*Anakuja kuihukumu dunia. Ataihukumu kwa uadilifu dunia inayokaliwa+Na mataifa kwa uaminifu wake.+

Maelezo ya Chini

Au “adhama.”
Au “Mwabuduni.”
Au labda, “kwa sababu ya fahari ya utakatifu wake.”
Au “kutikiswa.”
Au “Ataamua kesi ya.”
Au “amekuja.”