Zaburi 97:1-12

  • Yehova amekwezwa juu ya miungu mingine

    • “Yehova amekuwa Mfalme!” (1)

    • Mpendeni Yehova, chukieni maovu (10)

    • Nuru kwa ajili ya mwadilifu (11)

97  Yehova amekuwa Mfalme!+ Dunia na iwe na shangwe.+ Na visiwa vyake vingi vishangilie.+   Mawingu na giza zito vinamzunguka;+Uadilifu na haki ndio msingi wa kiti chake cha ufalme.+   Moto hutangulia mbele zake+Na kuwateketeza kabisa maadui wake pande zote.+   Umeme wake wa radi huiangazia nchi;Dunia huona na kutetemeka.+   Milima huyeyuka kama nta mbele za Yehova,+Mbele za Bwana wa dunia yote.   Mbingu hutangaza uadilifu wake,Na mataifa yote huona utukufu wake.+   Wote wanaoabudu sanamu yoyote ya kuchongwa na waaibishwe,+Wale wanaojigamba kuhusu miungu yao ya ubatili.+ Mwinamieni,* enyi miungu yote.+   Sayuni husikia na kufurahi;+Miji ya Yuda ina* shangweKwa sababu ya hukumu zako, Ee Yehova.+   Kwa maana wewe, Ee Yehova, ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote;Umekwezwa juu zaidi ya miungu mingine yote.+ 10  Enyi mnaompenda Yehova, chukieni maovu.+ Anaulinda uhai wa* washikamanifu wake;+Huwaokoa kutoka katika mkono wa* mwovu.+ 11  Nuru imemwangazia mwadilifu+Na shangwe walio wanyoofu moyoni. 12  Shangilieni kwa sababu ya Yehova, enyi waadilifu,Na mlishukuru jina lake takatifu.*

Maelezo ya Chini

Au “Mwabuduni.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda wana.”
Au “nafsi za.”
Tnn., “nguvu za.”
Tnn., “muushukuru ukumbusho wake.”