Zaburi 99:1-9

  • Yehova ni Mfalme mtakatifu

    • Ameketi kwenye kiti cha ufalme juu ya makerubi (1)

    • Mungu anayesamehe na kuadhibu (8)

99  Yehova amekuwa Mfalme.+ Mataifa na yatetemeke. Anaketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi.+ Dunia na itikisike.   Yehova ni mkuu Sayuni,Naye yuko juu ya mataifa yote.+   Na walisifu jina lako kuu,+Kwa maana linaogopesha, nalo ni takatifu.   Yeye ni mfalme hodari anayependa haki.+ Umeimarisha kabisa mambo manyoofu. Umetekeleza haki na uadilifu+ katika Yakobo.   Mkwezeni Yehova Mungu wetu+ na kuinama chini* mbele ya kiti cha miguu yake;+Yeye ni mtakatifu.+   Musa na Haruni walikuwa miongoni mwa makuhani wake,+Na Samweli alikuwa miongoni mwa wale walioliita jina lake.+ Walikuwa wakimwita Yehova,Naye alikuwa akiwajibu.+   Alikuwa akiongea nao kutoka katika nguzo ya wingu.+ Walishika vikumbusho vyake na amri aliyowapa.+   Ee Yehova Mungu wetu, uliwajibu.+ Ulikuwa Mungu uliyewasamehe,+Lakini uliwaadhibu* kwa sababu ya dhambi walizotenda.+   Mkwezeni Yehova Mungu wetu+Na mwiname chini* mbele ya mlima wake mtakatifu,+Kwa maana Yehova Mungu wetu ni mtakatifu.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “katikati ya.”
Au “kuabudu.”
Tnn., “ulilipiza kisasi.”
Au “mwabudu.”