Zekaria 12:1-14

  • Yehova atalinda Yuda na Yerusalemu (1-9)

    • Yerusalemu, “jiwe zito” (3)

  • Wamlilia waliyemdunga (10-14)

12  Tangazo: “Neno la Yehova kuhusu Israeli,” asema Yehova,Yule aliyezitandaza mbingu,+Aliyeweka msingi wa dunia,+Na kuumba roho* iliyo ndani ya mwanadamu.  “Tazama, ninafanya jiji la Yerusalemu liwe kikombe kinachosababisha* mataifa yote jirani yapepesuke; na jiji la Yuda litazingirwa, na pia Yerusalemu.+  Siku hiyo nitafanya Yerusalemu liwe jiwe zito* kwa mataifa yote. Kwa hakika wote watakaolinyanyua watajeruhiwa vibaya;+ na mataifa yote duniani yatakusanyika kupigana na jiji hilo.+  Siku hiyo,” asema Yehova, “nitamtia hofu kila farasi na kumtia wazimu yule anayempanda. Nitaikazia macho nyumba ya Yuda, lakini nitampofusha kila farasi wa mataifa.  Na mashehe* wa Yuda watasema moyoni mwao, ‘Wakaaji wa Yerusalemu ni nguvu kwetu kwa sababu ya Yehova wa majeshi Mungu wao.’+  Siku hiyo nitawafanya mashehe wa Yuda wawe kama chungu cha moto kati ya kuni na kama mwenge unaowaka kati ya safu ya miganda iliyokatwa ya nafaka,+ nao watayateketeza mataifa yote jirani yaliyo upande wa kulia na wa kushoto;+ na jiji la Yerusalemu litakuwa tena na wakaaji mahali pake,* huko Yerusalemu.+  “Na Yehova atayaokoa kwanza mahema ya Yuda, ili umaridadi wa* nyumba ya Daudi na umaridadi wa* wakaaji wa Yerusalemu usizidi sana ule wa Yuda.  Siku hiyo Yehova atakuwa ulinzi kuwazunguka wakaaji wa Yerusalemu;+ siku hiyo yule anayejikwaa* kati yao atakuwa kama Daudi, na nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa Yehova anayetangulia mbele yao.+  Na siku hiyo, kwa hakika nitayaangamiza mataifa yote yatakayokuja kushambulia Yerusalemu.+ 10  “Nitamimina roho ya kibali na dua juu ya nyumba ya Daudi na juu ya wakaaji wa Yerusalemu, nao watamtazama yule waliyemchoma,+ watamwombolezea kwa sauti kama ambavyo wangemwombolezea mwana wa pekee; watamhuzunikia sana kama ambavyo wangemhuzunikia mwana mzaliwa wa kwanza. 11  Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makubwa Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika Nchi Tambarare ya Megido.+ 12  Na nchi itaomboleza kwa sauti, kila ukoo peke yake; ukoo wa nyumba ya Daudi peke yake, na wanawake wao peke yao; ukoo wa nyumba ya Nathani+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 13  ukoo wa nyumba ya Lawi+ peke yake, na wanawake wao peke yao; ukoo wa Washimei+ peke yake, na wanawake wao peke yao; 14  na koo zote zinazobaki, kila ukoo peke yake, na wanawake wao peke yao.

Maelezo ya Chini

Au “pumzi.”
Au “bakuli linalosababisha.”
Au “lenye kulemea.”
Shehe alikuwa mkuu wa kabila.
Au “mahali pake panapostahili.”
Au “fahari ya.”
Au “fahari ya.”
Au “aliye dhaifu zaidi.”