Zekaria 13:1-9

  • Sanamu na manabii wa uwongo waondolewa (1-6)

    • Manabii wa uwongo wataaibika (4-6)

  • Mchungaji atapigwa (7-9)

    • Theluthi ya watu kusafishwa (9)

13  “Siku hiyo kisima kitafunguliwa kwa ajili ya nyumba ya Daudi na wakaaji wa Yerusalemu ili kuwasafisha dhambi na uchafu.+  “Siku hiyo,” asema Yehova wa majeshi, “nitafuta majina ya sanamu kutoka nchini,+ nayo hayatakumbukwa tena; nami nitawaondoa kabisa manabii+ na pia roho ya uchafu kutoka nchini.  Na mtu akitoa unabii tena, baba yake na mama yake waliomzaa watamwambia, ‘Hutaishi, kwa sababu umesema uwongo katika jina la Yehova.’ Na baba yake na mama yake waliomzaa watamchoma kisu kwa sababu ya unabii wake.+  “Siku hiyo kila nabii ataonea aibu maono yake anapotabiri; nao hawatavaa vazi rasmi la manyoya+ ili kudanganya.  Naye atasema, ‘Mimi si nabii. Mimi ni mkulima, kwa sababu mtu fulani alininunua nilipokuwa kijana.’  Na mtu akimuuliza, ‘Majeraha haya uliyo nayo katikati ya mabega yako* yametoka wapi?’ atajibu, ‘Nilijeruhiwa katika nyumba ya rafiki zangu.’”*   “Ee upanga, amka umshambulie mchungaji wangu,+Mshambulie rafiki yangu,” asema Yehova wa majeshi. “Mpige mchungaji,+ acha kondoo watawanyike;*+Nami nitaugeuza mkono wangu dhidi ya watu wa hali ya chini.”   “Na katika nchi yote,” asema Yehova,“Theluthi mbili za watu zitaangamizwa na kutoweka;*Na theluthi moja itaachwa humo.   Na theluthi hiyo moja nitaipitisha motoni;Nami nitawasafisha kama fedha inavyosafishwa,Na kuwajaribu kama dhahabu inavyojaribiwa.+ Wataliitia jina langu,Nami nitawajibu. Nitasema, ‘Wao ni watu wangu,’+ Nao watasema, ‘Yehova ni Mungu wetu.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “katikati ya mikono yako.” Yaani, kifuani au mgongoni.
Au “wale wanaonipenda.”
Au “kundi la kondoo litawanyike.”
Au “zitakufa.”