Zekaria 2:1-13

  • Maono ya 3: Mtu mwenye kamba ya kupimia (1-13)

    • Yerusalemu litapimwa (2)

    • Yehova, “ukuta wa moto kulizunguka pande zote” (5)

    • Kugusa mboni ya jicho la Mungu (8)

    • Watu wa mataifa mengi watajiunga na Yehova (11)

2  Nami nikatazama juu na kumwona mtu akiwa na kamba ya kupimia+ mkononi mwake.  Kwa hiyo nikamuuliza: “Unaenda wapi?” Akanijibu: “Naenda kupima jiji la Yerusalemu, ili nijue upana wake na urefu wake.”+  Na tazama! malaika aliyekuwa akizungumza nami akaondoka, na malaika mwingine akaja kukutana naye.  Kisha akamwambia: “Kimbia ukamwambie yule kijana, ‘“Yerusalemu litakaliwa+ kama eneo la mashambani lililo wazi,* kwa sababu ya watu wengi na mifugo mingi iliyomo.+  Nitakuwa ukuta wa moto kulizunguka pande zote,”+ asema Yehova, “nami nitakuwa utukufu ndani yake.”’”+  “Njooni! Njooni! Kimbieni kutoka nchi ya kaskazini,”+ asema Yehova. “Kwa maana nimewatawanya kuelekea pepo nne za mbinguni,”*+ asema Yehova.  “Njoo, Ee Sayuni! Kimbia, wewe unayekaa na binti ya Babiloni.+  Kwa maana hivi ndivyo anavyosema Yehova wa majeshi, ambaye baada ya kutukuzwa* amenituma kwa mataifa yaliyokuwa yakiwapora ninyi:+ ‘Yeyote anayewagusa ninyi anaigusa mboni ya jicho langu.*+  Kwa maana sasa nitaupunga mkono wangu dhidi yao, nao watakuwa nyara kwa watumwa wao wenyewe.’+ Na hakika mtajua kwamba Yehova wa majeshi amenituma. 10  “Paza sauti kwa shangwe, Ee binti ya Sayuni;+ kwa maana ninakuja,+ nami nitakaa kati yako,”+ asema Yehova. 11  “Mataifa mengi yatajiunga na Yehova siku hiyo,+ nao watakuwa watu wangu; nami nitakaa kati yenu.” Nanyi mtalazimika kujua kwamba Yehova wa majeshi amenituma kwenu. 12  Yehova atamiliki Yuda kama fungu lake katika ardhi takatifu, naye atalichagua tena jiji la Yerusalemu.+ 13  Nyamazeni, enyi nyote wenye mwili,* mbele za Yehova, kwa maana anachukua hatua kutoka katika makao yake matakatifu.

Maelezo ya Chini

Yaani, ambalo halijazingirwa na kuta.
Tnn., “kwenye pande nne za mbingu.”
Tnn., “baada ya utukufu.”
Au “analigusa jicho langu.”
Au “wanadamu.”