Zekaria 3:1-10

  • Maono ya 4: Kuhani mkuu avishwa mavazi mengine (1-10)

    • Shetani ampinga Kuhani Mkuu Yoshua (1)

    • ‘Nitamleta mtumishi wangu anayeitwa Chipukizi!’ (8)

3  Naye akanionyesha kuhani mkuu Yoshua+ akiwa amesimama mbele ya malaika wa Yehova, na Shetani+ alikuwa amesimama kwenye mkono wa kulia wa Yoshua ili kumpinga.  Kisha malaika wa Yehova akamwambia Shetani: “Yehova na akukemee, ewe Shetani,+ naam, Yehova, ambaye amechagua Yerusalemu,+ na akukemee! Je, mtu huyu si gogo lililochomolewa motoni?”  Sasa Yoshua alikuwa amevaa mavazi machafu akiwa amesimama mbele ya malaika.  Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni mavazi yake machafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama! Nimefuta kosa lako,* nawe utavishwa mavazi bora.”*+  Basi nikasema: “Na avikwe kilemba safi kichwani.”+ Nao wakamvika kilemba safi kichwani na kumvisha mavazi; na malaika wa Yehova alikuwa amesimama karibu.  Kisha malaika wa Yehova akamwambia Yoshua:  “Yehova wa majeshi anasema hivi, ‘Ikiwa utatembea katika njia zangu na kutekeleza majukumu niliyokupa, utakuwa mwamuzi nyumbani mwangu+ na kuzitunza* nyua zangu; nami nitakuruhusu ufike mbele zangu, pamoja na hawa wanaosimama hapa.’  “‘Tafadhali sikiliza, Ee Kuhani Mkuu Yoshua, wewe pamoja na wenzako wanaoketi mbele yako, kwa maana wanaume hawa ni ishara; tazama! ninamleta mtumishi wangu+ anayeitwa Chipukizi!+  Tazama jiwe ambalo nimeweka mbele ya Yoshua! Jiwe hili moja lina macho saba; nami ninachonga maandishi juu yake,’ asema Yehova wa majeshi, ‘nami nitaondoa hatia ya nchi hiyo kwa siku moja.’+ 10  “‘Siku hiyo,’ asema Yehova wa majeshi, ‘kila mmoja wenu atamwalika jirani yake aje chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake.’”+

Maelezo ya Chini

Au “hatia yako.”
Au “majoho ya kifahari.”
Au “kusimamia; kulinda.”