Zekaria 7:1-14

  • Yehova awashutumu wanaofunga kwa unafiki (1-14)

    • “Je, kweli mlifunga kwa ajili yangu?” (5)

    • ‘Mtendeane kwa haki, upendo mshikamanifu, na huruma’ (9)

7  Na katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Yehova lilimjia Zekaria+ siku ya nne ya mwezi wa tisa, yaani, mwezi wa Kislevu.*  Watu wa Betheli walimtuma Shareza na Regem-meleki na wanaume wake ili wamwombe Yehova kibali,*  wawaulize hivi makuhani wa nyumba ya* Yehova wa majeshi na pia manabii: “Je, nilie katika mwezi wa tano+ na kujinyima chakula, kama vile ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi sana?”  Neno la Yehova wa majeshi likanijia tena, likisema:  “Waambie watu wote nchini na makuhani, ‘Mlipofunga na kulia kwa sauti katika mwezi wa tano na mwezi wa saba+ kwa miaka 70,+ je, kweli mlifunga kwa ajili yangu?  Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mkila na kunywa kwa ajili yenu wenyewe?  Je, hampaswi kutii maneno ambayo Yehova alitangaza kupitia manabii wa kale,+ wakati jiji la Yerusalemu na majiji yaliyolizunguka yalipokuwa na wakaaji na yalipokuwa na amani, na watu walipokaa Negebu na Shefela?’”  Neno la Yehova likamjia tena Zekaria, likisema:  “Yehova wa majeshi anasema hivi: ‘Hukumuni kwa haki ya kweli,+ na mtendeane kwa upendo mshikamanifu+ na rehema. 10  Msimpunje mjane wala yatima,*+ mgeni+ wala maskini;+ na katika mioyo yenu msipangiane njama za kutendeana uovu.’+ 11  Lakini waliendelea kukataa kusikiliza,+ wakageuza migongo yao kwa ukaidi,+ na kuziba masikio yao ili wasisikie.+ 12  Waliifanya mioyo yao iwe kama almasi*+ nao walikataa kutii sheria* na maneno ambayo Yehova wa majeshi aliwapa kwa roho yake kupitia manabii wa kale.+ Kwa hiyo Yehova wa majeshi akakasirika sana.”+ 13  “‘Kama vile ambavyo hawakunisikiliza nilipowaita,+ mimi pia sikuwasikiliza waliponiita,’+ asema Yehova wa majeshi. 14  ‘Nami niliwatawanya kwa kimbunga kotekote katika mataifa yote ambayo hawakuyajua,+ na nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao, hivi kwamba hakuna yeyote aliyeingia wala kutoka;+ kwa maana waliibadili nchi yenye kutamanika ikawa kitu cha kutisha.’”

Maelezo ya Chini

Tnn., “wautulize uso wa Yehova.”
Au “hekalu la.”
Tnn., “mtoto asiye na baba.”
Au labda, “jiwe gumu,” kama vile jiwe la msasa.
Au “mafundisho.”