Zekaria 9:1-17

  • Mungu ayahukumu mataifa jirani (1-8)

  • Kuja kwa mfalme wa Sayuni (9, 10)

    • Mfalme mnyenyekevu apanda juu ya punda (9)

  • Watu wa Yehova watawekwa huru (11-17)

9  Tangazo: “Neno la Yehova liko dhidi ya nchi ya Hadraki,Nalo linalenga* Damasko+—Kwa maana macho ya Yehova yanawaangalia wanadamu+Na makabila yote ya Israeli—   Na dhidi ya Hamathi,+ inayopakana nayo,Na dhidi ya majiji ya Tiro+ na Sidoni,+ kwa maana yana hekima nyingi.+   Jiji la Tiro lilijijengea boma.* Lilirundika fedha kama mavumbiNa dhahabu kama mavumbi barabarani.+   Tazama! Yehova atachukua mali za jiji hilo,Naye ataliangamiza jeshi lake baharini;+Na jiji hilo litateketezwa motoni.+   Jiji la Ashkeloni litaona jambo hilo na kuogopa;Gaza litahisi maumivu makali sana,Ekroni pia, kwa sababu tumaini lake limeaibishwa. Mfalme wa Gaza ataangamizwa,Na Ashkeloni halitakaliwa na watu.+   Mwanaharamu ataishi Ashdodi,Nami nitakikomesha kiburi cha Mfilisti.+   Nitaondoa vitu vyenye damu kutoka kinywani mwakeNa vitu vyenye kuchukiza kutoka katikati ya meno yake,Naye atabaki kwa ajili ya Mungu wetu;Naye atakuwa kama shehe* nchini Yuda,+Na Ekroni kama Myebusi.+   Nitapiga kambi nikiwa mlinzi wa nyumba yangu,+Hivi kwamba hakuna yeyote atakayeingia na hakuna yeyote atakayetoka;Na hakuna msimamizi wa watumwa* atakayeingia humo tena,+Kwa maana sasa nimeyaona* kwa macho yangu.   Shangilia sana, Ee binti ya Sayuni. Paza sauti kwa ushindi, Ee binti ya Yerusalemu. Tazama! Mfalme wako anakuja kwako.+ Yeye ni mwadilifu, analeta wokovu,*Ni mnyenyekevu+ na amepanda punda,Amepanda mwanapunda dume,* mwana wa punda jike.+ 10  Nitaondoa gari la vita EfraimuNa farasi kutoka Yerusalemu. Upinde wa vita utachukuliwa. Naye atatangaza amani kwa mataifa;+Utawala wake utaenea kutoka bahari mpaka bahariNa kutoka Mto Efrati mpaka kwenye miisho ya dunia.+ 11  Lakini wewe, Ee mwanamke, kwa damu ya agano lako,Nitawatoa wafungwa wako katika shimo lisilo na maji.+ 12  Rudini katika ngome, enyi wafungwa wenye tumaini.+ Leo ninakwambia,‘Nitakulipa fungu maradufu, ewe mwanamke.+ 13  Kwa maana nitampinda* Yuda kama upinde wangu. Nitamjaza Efraimu kwenye upinde,*Nami nitawaamsha wana wako, Ee Sayuni,Dhidi ya wana wako, Ee Ugiriki,Nami nitakufanya uwe kama upanga wa shujaa.’ 14  Itaonekana kwamba Yehova yupo pamoja nao,Na mshale wake utafyatuka kama radi. Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova atapiga pembe,+Naye atasonga mbele pamoja na dhoruba za upepo za kusini. 15  Yehova wa majeshi atawalinda,Nao watayameza na kuyatiisha mawe ya kombeo.+ Watakunywa na kupiga kelele, kana kwamba wamekunywa divai;Nao watajazwa kama bakuli,Kama pembe za madhabahu.+ 16  Yehova Mungu wao atawaokoa siku hiyoWakiwa kundi la watu wake;+Kwa maana watakuwa kama vito vya taji vinavyong’aa kwenye ardhi yake.+ 17  Jinsi wema wake ulivyo mwingi kwelikweli,+Na jinsi uzuri wake unavyovutia ajabu! Nafaka itawafanya vijana wanaume wanawiri,Na divai mpya itawafanya mabikira wanawiri.”+

Maelezo ya Chini

Tnn., “litapumzika.”
Au “ngome.”
Shehe alikuwa mkuu wa kabila.
Inaonekana ni mateso ya watu wake.
Au “mkandamizaji.”
Au “naye ni mshindi; na ameokolewa.”
Au “punda dume.”
Tnn., “nitamkanyaga.”
Yaani, kama mshale.