WIMBO NA. 113

Amani Tuliyo Nayo

Amani Tuliyo Nayo

(Yohana 14:27)

  1. 1. Tumsifu Yehova,

    Mwenye amani,

    Atakomesha vita,

    Kuwe amani.

    Mkuu wa amani,

    Ni Kristo Yesu.

    Kutakuwa amani,

    Atawalapo.

  2. 2. Tumeacha ghadhabu,

    Na chuki pia.

    Mapanga na mikuki,

    Tumebadili.

    Ili kuwe amani,

    Tutasamehe,

    Na kuishi pamoja,

    Kama “kondoo.”

  3. 3. Amani ya Yehova,

    Baraka kwetu.

    Tutii maagizo,

    Toka moyoni.

    Wengine na waone,

    Tuna amani.

    Hadi Ufalme uje,

    Kuwe amani.