WIMBO NA. 119

Lazima Tuwe na Imani

Lazima Tuwe na Imani

(Waebrania 10:38, 39)

  1. 1. Kale Yehova Mungu kasema,

    Kupitia manabii.

    Leo kupitia Mwana wake,

    Anasema: ‘Tubuni! ’

    (KORASI)

    Je, tuna imani kweli?

    Ni lazima tuijenge.

    Je, ni ya matendo kweli?

    Imani iokoayo nafsi.

  2. 2. Amri ya Yesu Kristo twatii,

    Ufalme tunatangaza.

    Tuutangaze ujumbe wake

    Utakaotimizwa.

    (KORASI)

    Je, tuna imani kweli?

    Ni lazima tuijenge.

    Je, ni ya matendo kweli?

    Imani iokoayo nafsi.

  3. 3. Tuna imani nayo ni ngao;

    Kamwe hatutaogopa.

    Tunavumilia tukijua,

    Wokovu u karibu.

    (KORASI)

    Je, tuna imani kweli?

    Ni lazima tuijenge.

    Je, ni ya matendo kweli?

    Imani iokoayo nafsi.