WIMBO NA. 129

Tutaendelea Kuvumilia

Tutaendelea Kuvumilia

(Mathayo 24:13)

  1. 1. Tunawezaje

    kuvumilia mikazo?

    Yesu katuwekea

    mfano mzuri.

    Ahadi za Mungu,

    alitafakari.

    (KORASI)

    Basi tuvumilie.

    Tulinde imani.

    Kwa kuwa Atupenda,

    Tutavumilia hadi mwisho.

  2. 2. Japo maisha

    yamejawa na uchungu;

    Twatafakari,

    Mfumo mpya wa Mungu.

    Tuwepo, tuone.

    Tumeazimia.

    (KORASI)

    Basi tuvumilie.

    Tulinde imani.

    Kwa kuwa Atupenda,

    Tutavumilia hadi mwisho.

  3. 3. Hatufi moyo

    Wala hatutaogopa.

    Tutumikie

    hadi mwisho ufikapo.

    Tuzidi kudumu,

    Mwisho u karibu.

    (KORASI)

    Basi tuvumilie.

    Tulinde imani.

    Kwa kuwa Atupenda,

    Tutavumilia hadi mwisho.