WIMBO NA. 142

Kushikilia Tumaini Letu

Kushikilia Tumaini Letu

(Waebrania 6:18, 19)

  1. 1. Kwa karne nyingi watu wako gizani.

    Kazi zao ubatili mtupu.

    Inazidi kuonekana wazi:

    Kujiokoa hawawezi.

    (KORASI)

    Mwimbieni na kushangilia!

    Ufalme wake unakaribia.

    Uovu ataufutilia;

    Tumaini letu twashikilia.

  2. 2. ‘Siku ya Mungu iko karibu sana! ’

    Tusilie, ‘Jamani hadi lini? ’

    Karibuni tutapata uhuru.

    Yehova Mungu msifuni.

    (KORASI)

    Mwimbieni na kushangilia!

    Ufalme wake unakaribia.

    Uovu ataufutilia;

    Tumaini letu twashikilia.