WIMBO NA. 46

Asante, Yehova

Asante, Yehova

(1 Wathesalonike 5:18)

  1. 1. Asante Yehova, siku kwa siku,

    Umetupa nuru ya ajabu.

    Asante kwa pendeleo la sala,

    Twaweza kukujia na shida.

  2. 2. Asante, Yehova, kwa Mwana wako,

    Aliyeushinda ulimwengu.

    Asante kwa kutupa maagizo.

    Hivyo twaepuka matatizo.

  3. 3. Asante Yehova kwa pendeleo,

    La kukutangaza wewe leo.

    Asante ole zote zitakwisha,

    Baraka za Ufalme zidumu.