WIMBO NA. 54

“Hii Ndiyo Njia”

“Hii Ndiyo Njia”

(Isaya 30:​20, 21)

  1. 1. Njia ya amani,

    Uliyoipata.

    Uliyofundishwa,

    Njia ya zamani.

    Njia ambayo Yesu

    Alifundisha.

    Njia ya amani

    Njia ya Yehova.

    (KORASI)

    Njia hii; njia ya uzima

    Usisite wala kupotoka!

    Mungu wetu atuagiza:

    ‘Pita hapa; kaza macho mbele.’

  2. 2. Njia ya upendo,

    Tunaifuata.

    Sauti ya Mungu,

    Inatuongoza.

    Upendo na wema;

    Anatuonyesha.

    Njia ya upendo;

    Inatuchochea.

    (KORASI)

    Njia hii; njia ya uzima

    Usisite wala kupotoka!

    Mungu wetu atuagiza:

    ‘Pita hapa; kaza macho mbele.’

  3. 3. Njia ya Uzima,

    Usikengeuke.

    Tumeipata

    Njia bora zaidi,

    Njia ya amani,

    Njia ya upendo,

    Njia ya uzima.

    Asante Yehova.

    (KORASI)

    Njia hii; njia ya uzima

    Usisite wala kupotoka!

    Mungu wetu atuagiza:

    ‘Pita hapa; kaza macho mbele.’