WIMBO NA. 57

Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

Kuwahubiria Watu wa Namna Zote

(1 Timotheo 2:4)

  1. 1. Twatamani kumwiga Yehova,

    Mungu asiye na ubaguzi.

    Ni mapenzi yake watu wote,

    Wapate uzima wa milele.

    (KORASI)

    Hatutazami sura;

    Wala hali za watu.

    Twatangazia wote ujumbe.

    Kwa kuwa twawajali,

    Twawakaribisha wote,

    Wawe rafiki za Yehova.

  2. 2. Haidhuru wapatikanapo,

    Wanavyoonekana mwanzoni.

    La muhimu, walivyo moyoni​—⁠

    Alivyo yule mtu wa ndani.

    (KORASI)

    Hatutazami sura;

    Wala hali za watu.

    Twatangazia wote ujumbe.

    Kwa kuwa twawajali,

    Twawakaribisha wote,

    Wawe rafiki za Yehova.

  3. 3. Yehova awapa wote fursa,

    Waache njia za ulimwengu.

    Tuna hamu kujulisha wengi,

    Basi tuwahubirie wote.

    (KORASI)

    Hatutazami sura;

    Wala hali za watu.

    Twatangazia wote ujumbe.

    Kwa kuwa twawajali,

    Twawakaribisha wote,

    Wawe rafiki za Yehova.