WIMBO NA 76

Unahisije?

Unahisije?

(Waebrania 13:15)

  1. 1. We‘ unahisije

    kuhusu kuhubiri?

    Kuwafundisha watu

    wanaopendezwa?

    Ujitahidipo

    Kutimiza huduma

    Na Yehova afanye

    kazi ya kukuza.

    (KORASI)

    Tuna shangwe, twafurahi

    kujitoa kikamili.

    Basi tumsifu Mungu.

    Daima dawamu.

  2. 2. We‘ unahisije

    wanaposikiliza?

    Wanapoitikia

    ujumbe wa kweli?

    Hata wakatae

    bado twautangaza.

    Twafurahi kuitwa kwa

    jina la Mungu.

    (KORASI)

    Tuna shangwe, twafurahi

    kujitoa kikamili.

    Basi tumsifu Mungu.

    Daima dawamu.

  3. 3. We‘ unahisije

    kuwa na pendeleo,

    Alilotupa Mungu

    la kumwakilisha?

    Tunajivunia

    kutangaza Ufalme

    Kuwatafuta watu

    wanaostahili.

    (KORASI)

    Tuna shangwe, twafurahi

    kujitoa kikamili.

    Basi tumsifu Mungu.

    Daima dawamu.