SOMO LA 13

Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu Mungu

Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu Mungu

Mungu ni upendo. Lakini kwa nini dini zinazodai kwamba zinamwakilisha Mungu zimefanya mambo mengi sana maovu? Ni kwa sababu dini hizo ni za uwongo; zinapotosha ukweli kumhusu Mungu. Zinapotoshaje ukweli kumhusu Mungu? Mungu anahisije kuhusu hilo? Naye atachukua hatua gani?

1. Mafundisho ya dini za uwongo yanapotoshaje ukweli kumhusu Mungu?

Dini za uwongo “[zimebadili] kweli ya Mungu kwa ajili ya uwongo.” (Waroma 1:25) Kwa mfano, dini nyingi hazifundishi wafuasi wake jina la Mungu. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba lazima watu walitumie jina la Mungu. (Waroma 10:13, 14) Jambo baya linapotokea, baadhi ya viongozi wa dini husema ni mapenzi ya Mungu. Lakini huo ni uwongo. Mungu hasababishi kamwe mambo maovu. (Soma Yakobo 1:13.) Inasikitisha kwamba uwongo wa dini umefanya iwe vigumu kwa watu kumpenda Mungu.

2. Matendo ya dini za uwongo yanapotoshaje ukweli kumhusu Mungu?

Dini za uwongo huwatendea watu kinyume cha mapenzi ya Yehova. Biblia inasema kwamba “dhambi [za dini za uwongo] zimekusanyika pamoja mpaka mbinguni.” (Ufunuo 18:5) Kwa karne nyingi, dini za uwongo zimejihusisha na siasa, zimeunga mkono vita na kusababisha vifo vya watu wengi sana. Baadhi ya viongozi wa dini huishi maisha ya kifahari kwa kuwalazimisha wafuasi wao watoe sadaka. Matendo hayo yanathibitisha kwamba hawamjui Mungu na kwamba hawapaswi kumwakilisha.​—Soma 1 Yohana 4:8.

3. Mungu anahisije kuhusu dini za uwongo?

Ikiwa wewe unakasirishwa na mambo ambayo dini za uwongo zinafanya, unafikiri Yehova anahisije? Anawapenda watu, lakini anakasirishwa na viongozi wa dini wanaopotosha ukweli kumhusu na kuwatendea vibaya wafuasi wao. Anaahidi kwamba dini za uwongo zitaharibiwa na ‘hazitapatikana tena.’ (Ufunuo 18:21) Hivi karibuni, Mungu ataziharibu dini zote za uwongo.​—Ufunuo 18:8.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi Mungu anavyohisi kuhusu dini za uwongo. Chunguza mambo ambayo dini hizo zimefanya, na pia kwa nini hilo halipaswi kukuzuia kujifunza kumhusu Yehova.

4. Si dini zote zinazokubalika machoni pa Mungu

Watu wengi wanaamini kwamba dini ni kama barabara mbalimbali zinazotuongoza kwa Mungu. Je, hilo ni kweli? Soma Mathayo 7:13, 14, kisha mzungumzie swali hili:

  • Biblia inasema nini kuhusu barabara inayoongoza kwenye uzima?

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Je, kweli Biblia inafundisha kwamba dini nyingi zinakubalika machoni pa Mungu?

5. Dini za uwongo hazionyeshi upendo wa Mungu

Dini zimepotosha ukweli kumhusu Mungu katika njia nyingi. Kwa mfano, jambo moja baya sana ambalo dini zimefanya ni kuunga mkono vita. Ili kuona mfano mmoja, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

  • Makanisa mengi yalichukua msimamo gani wakati wa Vita vya Pili vya Ulimwengu?

  • Una maoni gani kuhusu msimamo wa dini hizo?

Soma Yohana 13:34, 35 na 17:16. Kisha mzungumzie maswali haya:

  • Unafikiri Yehova anahisije dini zinapojihusisha katika vita?

  • Dini za uwongo zimesababisha mambo mengi mabaya. Kutokana na mambo uliyojionea, dini zimeshindwa kuiga upendo wa Mungu katika njia gani?

Dini za uwongo hazijaonyesha upendo wa Mungu

6. Mungu anataka kuwasaidia watu watoke katika dini za uwongo

Soma Ufunuo 18:4, a kisha mzungumzie swali hili:

  • Unahisije kujua kwamba Mungu anataka kuwasaidia watu watoke katika dini za uwongo?

7. Endelea kujifunza kumhusu Mungu wa kweli

Je, dini za uwongo zinapaswa kuathiri maoni yako kumhusu Mungu? Fikiria mtoto ambaye anakataa kufuata mwongozo wa hekima kutoka kwa baba yake. Mtoto huyo anaondoka nyumbani na kuishi maisha mapotovu. Baba yake haungi mkono matendo ya mtoto huyo. Kwa nini si sawa kumlaumu baba kwa sababu ya uasi wa mtoto wake?

  • Je, ni sawa kumlaumu Yehova na kuacha kujifunza kumhusu kwa sababu ya matendo ya dini za uwongo?

WATU FULANI HUSEMA: “Sipendi mambo ya Mungu kwa sababu dini zimesababisha matatizo mengi.”

  • Je, wewe unahisi hivyo?

  • Kwa nini matendo ya dini za uwongo hayapaswi kufanya uwe na maoni mabaya kumhusu Yehova?

MUHTASARI

Dini za uwongo zimepotosha ukweli kumhusu Mungu kupitia mafundisho yao ya uwongo na matendo yao ya kikatili. Mungu ataziharibu dini za uwongo.

Ungejibuje?

  • Una maoni gani kuhusu mambo ambayo dini za uwongo zinafundisha na matendo yao?

  • Yehova anahisije kuhusu dini za uwongo?

  • Mungu atachukua hatua gani dhidi ya dini za uwongo?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza njia mbili ambazo dini nyingi zinamkasirisha Mungu.

“Je, Dini Zote Ni Sawa? Je, Zote Zinaongoza kwa Mungu? (Makala iliyo kwenye mtandao)

Kwa nini Yehova anataka tumwabudu tukiwa pamoja na wengine?

“Je, Ni Lazima Mtu Awe Katika Dini Fulani?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Kasisi fulani alihangaishwa na dini yake. Lakini hilo halikumzuia kujifunza ukweli kumhusu Mungu.

“Kwa Nini Kasisi Alibadili Dini?” (Amkeni!, Februari 2015)

Kwa miaka mingi, dini zimefundisha uwongo unaofanya watu wafikiri kwamba Mungu hajali na ni mkatili. Jifunze ukweli kuhusu mambo matatu yaliyopotoshwa.

“Uwongo Unaofanya Watu Wasimpende Mungu” (Mnara wa Mlinzi, Novemba 1, 2013)

a Ili kujua kwa nini kitabu cha Ufunuo kinafafanua dini za uwongo kuwa mwanamke anayeitwa Babiloni Mkubwa, ona Maelezo ya Ziada 1.