SOMO LA 14

Ni Ibada Gani Inayokubalika kwa Mungu?

Ni Ibada Gani Inayokubalika kwa Mungu?

Kama somo lililotangulia lilivyoonyesha, si dini zote zinazokubalika machoni pa Mungu. Hata hivyo, tunaweza kumwabudu Muumba wetu kwa njia inayomfurahisha. Ni ‘namna gani ya ibada’ au dini inayokubalika kwake? (Yakobo 1:​27, maelezo ya chini) Chunguza mambo ambayo Biblia inafundisha.

1. Ibada yetu inapaswa kutegemea msingi gani?

Ibada yetu inapaswa kutegemea Biblia. Yesu alimwambia Mungu hivi: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Baadhi ya dini zinapuuza ukweli ulio katika Biblia, Neno la Mungu lililoongozwa na roho. Badala yake, wanafuata mafundisho na tamaduni za wanadamu. Lakini Yehova hafurahishwi na wale ‘wanaopuuza amri ya Mungu.’ (Soma Marko 7:9.) Hata hivyo, tunafanya moyo wake ushangilie tunaposhikamana na Biblia na kufuata ushauri wake.

2. Tunapaswa kumwabudu Yehova jinsi gani?

Tunapaswa kumwabudu Yehova peke yake kwa sababu yeye ndiye Muumba wetu. (Ufunuo 4:11) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kumpenda na kumwabudu yeye peke yake, bila kutumia sanamu, mifano, au picha.​—Soma Isaya 42:8.

Ibada yetu inapaswa kuwa “takatifu na yenye kukubalika” kwa Yehova. (Waroma 12:1) Hilo linamaanisha kwamba tunapaswa kuishi kulingana na viwango vyake vya maadili. Kwa mfano, wale wanaompenda Yehova wanapenda na kufuata viwango vyake kuhusu ndoa. Pia, wanaepuka mazoea yasiyofaa kama vile kuvuta sigara, kutumia dawa za kulevya au kunywa pombe kupita kiasi. a

3. Kwa nini tunapaswa kumwabudu Yehova pamoja na waamini wenzetu?

Mikutano tunayofanya kila juma hutupatia fursa ya ‘kumsifu Yehova katika kutaniko.’ (Zaburi 111:1, 2) Njia moja ambayo tunamsifu Mungu ni kwa kumwimbia nyimbo za sifa. (Soma Zaburi 104:33.) Yehova anataka tuhudhurie mikutano kwa sababu anatupenda na anajua kwamba itatusaidia tufurahie maisha milele. Tunapohudhuria mikutano tunatiwa moyo, na tunawatia moyo wengine.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza kwa nini Yehova hataki tutumie sanamu katika ibada. Jifunze njia mbalimbali tunazoweza kumsifu Mungu.

4. Hatupaswi kutumia sanamu katika ibada yetu

Tunajuaje kwamba Mungu hataki tutumie sanamu katika ibada? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

  • Nyakati za Biblia, ni nini kilichowapata watu wa Mungu walipomwabudu kwa kutumia sanamu?

Watu fulani hutumia sanamu kumwabudu Mungu ili wajihisi wakiwa karibu naye. Je, hilo linaweza kufanya Mungu akatae ibada yao? Soma Kutoka 20:4-6 na Zaburi 106:35, 36, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Umeona watu wakitumia sanamu na mifano gani katika ibada?

  • Yehova anahisije kuhusu kutumia sanamu?

  • Unahisije kuhusu kutumia sanamu katika ibada?

5. Tukimwabudu Yehova peke yake tutakuwa huru kutoka kwenye mafundisho ya uwongo

Ona jinsi kumwabudu Yehova kwa njia inayokubalika kunavyoweza kutuweka huru kutoka kwenye mafundisho ya uwongo. Onyesha VIDEO.

Soma Zaburi 91:14, kisha mzungumzie swali hili:

  • Yehova anaahidi kutufanyia nini tunapoonyesha kwamba tunampenda kwa kumwabudu yeye peke yake?

6. Tunamwabudu Mungu katika mikutano ya kutaniko

Tunamsifu Yehova na kutiana moyo kwa kuimba na kutoa maelezo katika mikutano ya kutaniko. Soma Zaburi 22:22, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, unafurahia kusikiliza maelezo ya wengine mikutanoni?

  • Je, ungependa kujitayarisha ili utoe maelezo?

7. Yehova anafurahi tunapowaambia wengine mambo tunayojifunza

Kuna njia nyingi tunazoweza kutumia ili kuwaambia wengine kweli za Biblia. Soma Zaburi 9:1 na 34:1, kisha mzungumzie swali hili:

  • Ni jambo gani ulilojifunza katika Biblia ambalo ungependa kuwaambia watu wengine?

WATU FULANI HUSEMA: “Haiwezekani kumfurahisha Mungu.”

  • Wewe una maoni gani?

MUHTASARI

Tunamfurahisha Muumba wetu kwa kumwabudu yeye peke yake, kwa kumsifu katika mikutano ya kutaniko, na kuwaeleza wengine mambo tunayojifunza.

Ungejibuje?

  • Tunawezaje kujifunza jinsi ya kumwabudu Mungu kwa njia inayokubalika?

  • Kwa nini tunapaswa kumwabudu Yehova peke yake?

  • Kwa nini tunapaswa kuabudu pamoja na watu wengine wanaotaka kumfurahisha Mungu?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Katika simulizi “Situmikii Sanamu Tena,” soma uone kwa nini mwanamke fulani aliacha kutumia sanamu katika ibada.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2011)

Jifunze kuhusu mambo yanayoweza kukusaidia utoe maelezo kwenye mikutano ya kutaniko.

“Msifu Yehova Katika Kutaniko” (Mnara wa Mlinzi, Januari 2019)

Ona jinsi kijana fulani alivyonufaika kwa kuhudhuria mikutano ya kutaniko ingawa haikuwa rahisi kwake.

Yehova Alinitunza (3:07)

Wengi wanaamini kwamba msalaba ni ishara ya Ukristo. Je, tunapaswa kuutumia katika ibada yetu?

“Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumii Msalaba Katika Ibada?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

a Habari hizo zitazungumziwa zaidi baadaye katika kitabu hiki.