Biblia inasema kwamba maisha ya wanadamu ni ‘mafupi na yamejaa taabu.’ (Ayubu 14:1) Je, Mungu anataka tuwe na maisha kama hayo? Ikiwa sivyo, ana kusudi gani kwa wanadamu? Je, kusudi hilo litatimizwa? Chunguza majibu yenye kufariji yanayopatikana katika Biblia.
1. Yehova anataka tuishi maisha ya aina gani?
Yehova anataka tuwe na maisha bora kabisa. Alipowaumba wanadamu wa kwanza Adamu na Hawa, aliwaweka katika paradiso maridadi, bustani ya Edeni. Kisha “Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia: ‘Zaeni, muwe wengi, muijaze dunia na kuitiisha.’” (Mwanzo 1:28) Yehova alitaka wapate watoto, waifanye dunia nzima kuwa paradiso na kuwatunza wanyama. Alikusudia kwamba watu wote wawe na afya kamilifu na waishi milele.
Ingawa mambo ni tofauti leo,a kusudi la Mungu halijabadilika. (Isaya 46:10, 11) Bado anataka wanadamu watiifu waishi milele katika hali kamilifu.—Soma Ufunuo 21:3, 4.
2. Tunawezaje kuwa na maisha yenye kusudi leo?
Yehova alituumba tukiwa na ‘uhitaji wa kiroho,’ yaani, tamaa ya kumjua na kumwabudu. (Soma Mathayo 5:3-6.) Anataka tuwe na urafiki wa karibu pamoja naye, ‘tutembee katika njia zake zote, tumpende,’ na kumtumikia ‘kwa moyo wetu wote.’ (Kumbukumbu la Torati 10:12; Zaburi 25:14) Tunapofanya hivyo, tunakuwa na furaha ya kweli hata ingawa tunakabili matatizo. Tunapomwabudu Yehova, maisha yetu yanakuwa na kusudi la kweli kwa sababu tunaishi kulingana na viwango vyake.
CHIMBA ZAIDI
Jifunze kuhusu upendo mkubwa ambao Yehova alionyesha alipoumba dunia kwa ajili ya wanadamu na kile ambacho Neno lake linasema kuhusu kusudi la uhai.
3. Yehova anataka wanadamu wafurahie maisha yenye kusudi