SOMO LA 28

Onyesha Shukrani kwa Mambo Ambayo Yehova na Yesu Wamekufanyia

Onyesha Shukrani kwa Mambo Ambayo Yehova na Yesu Wamekufanyia

Unahisije rafiki yako anapokupatia zawadi nzuri? Bila shaka, unafurahi sana na unataka kumwonyesha rafiki yako kwamba unaithamini zawadi hiyo. Yehova na Yesu walitupatia zawadi bora kuliko zawadi zote. Ni zawadi gani hiyo, na tunaweza kuonyeshaje kwamba tunaithamini?

1. Ni kwa njia gani tunaweza kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo Mungu na Kristo wametufanyia?

Biblia inatuahidi kwamba “kila mtu anayemwamini [Yesu]” anaweza kuishi milele. (Yohana 3:16) Hilo linamaanisha nini? Kumwamini Yesu kunahusisha mengi. Tunahitaji kuonyesha imani yetu kupitia maamuzi na matendo yetu. (Yakobo 2:17) Tunapoonyesha imani kupitia matendo na maneno yetu, tunaimarisha urafiki wetu na Yesu na pia Yehova, Baba yake.​—Soma Yohana 14:21.

2. Ni tukio gani la pekee linalotupatia fursa ya kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo Yehova na Yesu wametufanyia?

Usiku kabla ya kifo chake, Yesu aliwaambia wafuasi wake njia nyingine ya kuonyesha shukrani kwa dhabihu yake. Alianzisha tukio la pekee ambalo Biblia inaliita “Mlo wa Jioni wa Bwana,” au Ukumbusho wa Kifo cha Kristo. (1 Wakorintho 11:20) Yesu alianzisha tukio hilo ili mitume wake na Wakristo wote wa kweli wakumbuke kwamba alitoa uhai wake kwa ajili yetu. Yesu aliamuru hivi kuhusu tukio hilo: “Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka.” (Luka 22:19) Unapohudhuria Ukumbusho, unaonyesha shukrani kwa upendo mkubwa ambao Yehova na Yesu wametuonyesha.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza njia nyingine ambazo tunaweza kuonyesha shukrani kwa upendo mkubwa ambao Yehova na Yesu wametuonyesha. Jifunze kwa nini Ukumbusho wa kifo cha Kristo ni muhimu.

3. Tunaonyesha shukrani kupitia matendo

Wazia kwamba mtu fulani alikuokoa ili usizame ndani ya maji. Je, unaweza kusahau jambo ambalo mtu huyo alikufanyia? Au je, utatafuta njia za kumwonyesha shukrani kwa jambo alilokufanyia?

Yehova ndiye chanzo cha uhai wetu. Soma 1 Yohana 4:8-10, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Kwa nini dhabihu ya Yesu ni zawadi ya pekee?

  • Unahisije kuhusu mambo ambayo Yehova na Yesu wamekufanyia?

Tunaweza kuonyeshaje shukrani kwa mambo ambayo Yehova na Yesu wametufanyia? Soma 2 Wakorintho 5:15 na 1 Yohana 4:11; 5:3. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

  • Kulingana na andiko hilo, tunawezaje kuonyesha shukrani?

4. Mwige Yesu

Njia nyingine ya kuonyesha shukrani ni kumwiga Yesu. Soma 1 Petro 2:21, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unaweza kufuata hatua za Yesu kwa ukaribu jinsi gani?

5. Hudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo

Ili uone jambo lililotokea Yesu alipoanzisha Mlo wa Jioni wa Bwana, soma Luka 22:14, 19, 20. Kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ni nini kilichotokea wakati wa Mlo wa Jioni wa Bwana?

  • Ni nini kinachowakilishwa na mkate na divai?​—Ona mstari wa 19 na 20.

Yesu alitaka wanafunzi wake waadhimishe Mlo wa Jioni wa Bwana mara moja kwa mwaka, katika tarehe inayolingana na siku ya kifo chake. Hivyo, Mashahidi wa Yehova hukutana kila mwaka ili kukumbuka kifo cha Kristo wakifuata njia aliyoagiza. Ili ujifunze kuhusu mkutano huu muhimu, onyesha VIDEO. Kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: Kumbuka Kifo cha Yesu (1:42)

  • Ni nini hufanyika wakati wa Ukumbusho?

Mkate na divai ni mifano. Mkate unawakilisha mwili mkamilifu wa kibinadamu wa Yesu ambao aliutoa uwe dhabihu kwa ajili yetu. Divai inawakilisha damu yake

WATU FULANI HUSEMA: “Ili uokolewe unahitaji tu kumwamini Yesu.”

MUHTASARI

Tunaonyesha shukrani kwa mambo ambayo Yesu ametufanyia kwa kumwamini, na kuhudhuria Ukumbusho wa kifo chake.

Ungejibuje?

  • Kumwamini Yesu kunamaanisha nini?

  • Ni kwa njia gani unaweza kuonyesha shukrani kwa mambo ambayo Yehova na Yesu wamekufanyia?

  • Kwa nini ni muhimu sana kuhudhuria Ukumbusho wa kifo cha Kristo?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Kifo cha Kristo hutuchochea kufanya nini?

Aliutumia Mwili Wake Kumheshimu Yehova (9:30)

Jifunze mengi kuhusu imani na jinsi ya kuionyesha.

“Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova” (Mnara wa Mlinzi, Oktoba 2016)

Katika simulizi “Ninajihisi Nikiwa Safi, Mzima, na Ninafurahia Kuwa Hai,” ona jinsi maisha ya mwanamke fulani yalivyobadilika baada ya kujifunza kuhusu dhabihu ya Kristo.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Agosti 1, 2011)

Ona kwa nini ni watu wachache wanaokula mkate na kunywa divai wakati wa Ukumbusho.

“Kwa Nini Mashahidi wa Yehova Wanaadhimisha Mlo wa Jioni wa Bwana kwa Njia Tofauti na Dini Nyingine?” (Makala iliyo kwenye mtandao)