SOMO LA 33

Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?

Ufalme wa Mungu Utatimiza Nini?

Tayari Ufalme wa Mungu umeanza kutawala. Hivi karibuni utafanya mabadiliko makubwa duniani. Tutachunguza baadhi ya mambo mazuri ambayo tunatazamia kufurahia chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu.

1. Ufalme wa Mungu utaletaje amani na haki duniani?

Yesu, Mfalme wa Ufalme wa Mungu, atawaangamiza watu waovu na serikali zote katika vita vya Har–​Magedoni. (Ufunuo 16:14, 16) Wakati huo, ahadi hii ya Biblia itatimizwa kikamili: “Bado muda mfupi tu, na watu waovu hawatakuwepo tena.” (Zaburi 37:10) Kupitia Ufalme huo, Yesu atahakikisha kwamba kuna amani na haki duniani pote.​—Soma Isaya 11:4.

2. Maisha yatakuwaje mapenzi ya Mungu yatakapotimizwa duniani?

Chini ya utawala wa Ufalme wa Mungu, “waadilifu wataimiliki dunia, nao wataishi humo milele.” (Zaburi 37:29) Wazia kuishi katika ulimwengu ambao kila mtu ni mwadilifu, watu wote wanampenda Yehova na wanapendana! Watu hawatakuwa wagonjwa tena, na kila mtu ataishi milele.

3. Ufalme wa Mungu utatimiza nini baada ya waovu kuangamizwa?

Baada ya waovu kuangamizwa, Yesu atatawala akiwa Mfalme kwa miaka elfu moja. Wakati huo, Yesu na watawala wenzake 144,000 watawasaidia wanadamu walio duniani kuwa wakamilifu na wasio na dhambi. Mwishoni mwa kipindi hicho, dunia itakuwa paradiso maridadi, na watu wote watakuwa na furaha kwa sababu ya kutii sheria za Yehova. Kisha Yesu atamrudishia utawala Yehova Baba yake. Wakati huo, ‘jina la Yehova litakuwa limetakaswa’ kikamili. (Mathayo 6:9, 10) Yehova atakuwa amethibitika kuwa Mtawala mzuri anayewajali raia wake. Kisha Yehova atamwangamiza Shetani, roho waovu, na watu wengine watakaoasi utawala wa Mungu. (Ufunuo 20:7-10) Hali kamilifu zitakazoletwa na Ufalme wa Mungu zitadumu milele.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza kwa nini tunaweza kuamini kwamba Mungu atatumia Ufalme kutimiza ahadi zote zilizo katika Biblia kuhusu wakati ujao.

4. Ufalme wa Mungu utakomesha serikali za wanadamu

“Mwanadamu amemtawala mwanadamu mwenzake kwa kumuumiza.” (Mhubiri 8:9) Kupitia Ufalme wake, Yehova ataondoa ukosefu huo wa haki.

Soma Danieli 2:44 na 2 Wathesalonike 1:6-8, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yehova na Mwana wake, Yesu, watachukua hatua gani dhidi ya serikali za wanadamu na wale wanaoziunga mkono?

  • Mambo ambayo umejifunza kumhusu Yehova na Yesu yanakuhakikishiaje kwamba watatenda kwa haki na bila upendeleo?

5. Yesu ndiye Mfalme bora

Akiwa Mfalme wa Ufalme wa Mungu, Yesu atafanya mambo mengi ili kuwasaidia raia wake. Onyesha VIDEO ili uone kwamba Yesu amethibitisha anatamani kuwasaidia watu na Mungu amempa nguvu za kufanya hivyo.

Yesu alipokuwa duniani, alionyesha mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza. Kati ya baraka zilizoonyeshwa, ni baraka gani unayotazamia kwa hamu? Soma Maandiko yaliyoonyeshwa ili kujifunza mengi kuhusu baraka hizo.

YESU ALIPOKUWA DUNIANI . . .

YESU AKIWA MBINGUNI . . .

  • alikuwa na nguvu za kudhibiti hali ya hewa.​—Marko 4:36-41.

  • atahakikisha watu wote wana afya kamilifu.​—Isaya 33:24.

6. Ufalme wa Mungu utaleta wakati ujao ulio bora

Ufalme wa Mungu utatimiza kikamili kusudi ambalo Yehova alikuwa nalo mwanzoni kuelekea wanadamu. Wanadamu wataishi milele katika paradiso duniani. Onyesha VIDEO ili uone jinsi Yehova anavyomtumia Mwana wake, Yesu, kutimiza kusudi lake.

Soma Zaburi 145:16, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unahisije kujua kwamba Yehova “[atatosheleza] tamaa ya kila kitu kilicho hai”?

WATU FULANI HUSEMA: “Ikiwa wanadamu wote watashirikiana, tunaweza kutatua matatizo ulimwenguni.”

  • Ufalme wa Mungu utatatua matatizo gani ambayo serikali za wanadamu zimeshindwa kutatua?

MUHTASARI

Ufalme wa Mungu utatimiza malengo yake yote. Utaifanya dunia yote kuwa paradiso iliyojaa watu wema watakaomwabudu Yehova milele.

Ungejibuje?

  • Ufalme wa Mungu utalitakasaje jina la Yehova?

  • Kwa nini tunaweza kuamini kwamba Ufalme wa Mungu utatimiza ahadi zilizo katika Biblia?

  • Ni jambo gani unalotazamia kwa hamu kati ya mambo ambayo Ufalme wa Mungu utatimiza?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze maana ya Har–Magedoni.

“Vita vya Har–Magedoni Ni Nini?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Chunguza kile kitakachotukia wakati utawala wa miaka elfu moja wa Yesu na baada ya hapo.

“Ni Nini Kitakachotokea Katika Siku ya Hukumu?” (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2012)

Ona jinsi familia zinavyoweza kutafakari pamoja kuhusu baraka za wakati ujao za Ufalme wa Mungu.

Jiwazie Ukiwa Katika Paradiso (1:50)

Katika makala “Nilikuwa na Maswali Mengi Yaliyonisumbua,” ona jinsi mwasi wa kisiasa alivyopata majibu ya maswali yaliyokuwa yakimhangaisha.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Januari 1, 2012)