SEHEMU YA 13

Tunapaswa Kufanya Nini ili Kumpendeza Mungu?

Tunapaswa Kufanya Nini ili Kumpendeza Mungu?

Epuka mambo mabaya. 1 Wakorintho 6:9, 10

Ikiwa tunampenda Yehova, hatutafanya mambo ambayo anachukia.

Yehova hataki tuibe, tulewe, au tutumie dawa za kulevya.

Mungu anachukia kuua, kutoa mimba, na ngono kati ya watu wa jinsia moja. Hataki tuwe wenye pupa au tupigane na wengine.

Hatupaswi kuabudu sanamu wala kuwasiliana na roho waovu.

Katika dunia itakayokuwa Paradiso, hakutakuwa na watu wanaofanya mabaya.

Fanya mema. Mathayo 7:12

Ili tumpendeze Mungu, tunapaswa kujitahidi kuwa kama yeye.

Waonyeshe wengine upendo kwa kuwa mwenye fadhili na mkarimu.

Uwe mnyoofu.

Uwe mwenye rehema na mwenye kusamehe.

Waambie wengine kumhusu Yehova na njia zake.​—Isaya 43:10.