Mungu wa kweli aliwaongoza wanaume fulani kuandika mawazo yake katika kitabu kimoja kitakatifu. Kitabu hicho ni Biblia. Biblia ina habari muhimu ambazo Mungu anataka uzijue.
Mungu anajua mambo yanayotufaa zaidi, na yeye ndiye Chanzo cha hekima yote. Ukimsikiliza, utapata hekima ya kweli.—Methali 1:5.
Mungu anataka kila mtu duniani asome Biblia. Inapatikana katika lugha nyingi leo.
Ikiwa unataka kumsikiliza Mungu, ni lazima usome Biblia na kuielewa.
Ulimwenguni pote, Mashahidi wa Yehova wanajulikana kwa kuwa na programu ya kuwafundisha watu Biblia bila malipo. Jionee jinsi funzo hilo linavyoongozwa.