SEHEMU YA 3

Maisha Yalikuwaje Katika Paradiso?

Maisha Yalikuwaje Katika Paradiso?

Yehova aliwapa Adamu na Hawa vitu vingi vizuri. Mwanzo 1:28

Yehova alimuumba mwanamke wa kwanza, Hawa, na akampa Adamu mwanamke huyo awe mke wake.—Mwanzo 2:21, 22.

Yehova aliwaumba wakiwa na akili na miili mikamilifu, bila kasoro yoyote.

Waliishi katika bustani ya Edeni iliyokuwa Paradiso, bustani hiyo maridadi sana ilikuwa na mto, miti ya matunda, na wanyama.

Yehova alizungumza nao; akawafundisha. Ikiwa wangemsikiliza, wangeishi milele katika Paradiso duniani.

Mungu aliwaambia wasile matunda ya mti mmoja. Mwanzo 2:16, 17

Yehova aliwaonyesha Adamu na Hawa mti mmoja wa matunda katika bustani na kuwaambia kwamba kama wangekula matunda ya mti huo, wangekufa.

Malaika mmoja alimwasi Mungu. Malaika huyo mwovu anaitwa Shetani Ibilisi.

Shetani hakutaka Adamu na Hawa wamtii Yehova. Hivyo, akatumia nyoka kumwambia Hawa kwamba akila matunda ya mti huo, hatakufa, bali atakuwa kama Mungu. Lakini huo ulikuwa uwongo mtupu.—Mwanzo 3:1-5.