SEHEMU YA 14

Unawezaje Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova?

Unawezaje Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova?

Amua kuwa upande wa Mungu. 1 Petro 5:6-9

Epuka desturi zozote zinazopingana na Biblia. Unahitaji ujasiri ili kufanya hivyo.

Usijiingize katika siasa za mataifa; mataifa hayo hayaungi mkono Yehova na Ufalme wake.

Fanya uamuzi mzuri​—msikilize Mungu. Mathayo 7:24, 25

Shirikiana na Mashahidi wa Yehova; nao watakusaidia kumkaribia Mungu.

Endelea kujifunza kumhusu Mungu na ujitahidi kutii amri zake.

Imani yako itakapokuwa yenye nguvu zaidi, ujiweke wakfu kwa Yehova na ubatizwe.​—Mathayo 28:19.

Msikilize Mungu. Soma Biblia, na uwaombe Mashahidi wa Yehova wakusaidie kuielewa. Kisha, ufanye mambo unayojifunza. Ukifanya hivyo, utaishi milele.​—Zaburi 37:29.