SEHEMU YA 7

Yesu Alikuwa Nani?

Yesu Alikuwa Nani?

Yehova alimtuma Yesu duniani. 1 Yohana 4:9

Ikiwa tunataka kumpendeza Yehova, ni lazima tumsikilize mtu mwingine wa maana sana. Muda mrefu kabla ya kumuumba Adamu, Yehova alimuumba kiumbe wa roho mwenye nguvu sana mbinguni.

Baadaye, Yehova alimtuma azaliwe huko Bethlehemu na bikira aliyeitwa Maria. Mtoto huyo akapewa jina, Yesu.—Yohana 6:38.

Akiwa mwanadamu duniani, Yesu alionyesha sifa za Mungu kikamili. Alikuwa mwenye fadhili, upendo, na mwenye kufikika. Aliwafundisha wengine kweli kumhusu Yehova bila woga.

Yesu alitenda mema lakini alichukiwa. 1 Petro 2:21-24

Yesu pia aliponya wagonjwa na akawafufua wafu.

Viongozi wa kidini walimchukia Yesu kwa sababu alifunua mafundisho yao ya uwongo na njia zao mbovu.

Viongozi wa kidini waliwachochea Waroma wampige Yesu na kumuua.