Yesu alisema watu wenye mioyo minyoofu watatambua kweli wanapoisikia. (Yoh. 10:4, 27) Kwa hiyo, kila tunapozungumza na watu tunahitaji kuwaeleza kweli rahisi zinazopatikana katika Biblia. Jaribu kuanza kwa kuuliza hivi: “Je, unajua kwamba . . . ?” au “Umewahi kusikia kwamba . . . ?” Kisha tumia Biblia kufafanua kweli hiyo. Kweli rahisi ya Biblia inaweza kupanda mbegu katika moyo wa mtu, na Mungu anaweza kuikuza mbegu hiyo!—1 Kor. 3:6, 7.