WIMBO NA. 111

Sababu za Kuwa na Shangwe

Sababu za Kuwa na Shangwe

(Mathayo 5:12)

  1. 1. Tuna sababu nyingi sana,

    Kuwa na shangwe halisi.

    Watu wa mataifa yote,

    Wanajiunga na sisi.

    Tunashangilia moyoni,

    Neno linaeleweka.

    Tunajifunza kila siku;

    Imani yaongezeka.

    Nayo shangwe yetu yazidi,

    Kama moto uwakao.

    Ingawa tuna matatizo,

    Kwetu Yehova ni ngao.

    (KORASI)

    Yehova ni shangwe yetu,

    Kazi zake za ajabu.

    Mawazo yake yapita yetu,

    Mungu mwema na mkuu!

  2. 2. Tunaziona kazi zake,

    Mbingu, bahari, dunia.

    Anastahili kusifiwa,

    Kwa kazi za uumbaji.

    Sasa twatangaza ushindi,

    Wa Ufalme wa Yehova.

    Ujumbe wa baraka zake,

    Kotekote twatangaza.

    Siku mpya yakaribia,

    Sikuzote kuwe shangwe.

    Dunia nazo mbingu mpya,

    Milele tushangilie.

    (KORASI)

    Yehova ni shangwe yetu,

    Kazi zake za ajabu.

    Mawazo yake yapita yetu,

    Mungu mwema na mkuu!